Header Ads

RAIS MKAPA AZINDUA THE GLOBAL BUSSINESS ROUNDTABLE




Na Happiness Katabazi
RAIS Mstaafu Benjamin Mkapa amewaasa wanataaluma, wafanyabiashara na wote wanaomwamini Mwenyezi Mungu  hapa nchini kuketi pamoja na kujadiliana na kushauri ni mbinu gani zitumike ili ziweze kuwainua wafanyabiashara wadogo hususani katika sekta ya Kilimo.

Rais Mkapa alitoa rai hiyo juzi usiku wakati alipokuwa anazindua rasmi utekelezwaji wa kuanza kutumika kwa taasisi ya The Global Bussiness Roundtable (GBR) yenye makao makao makuu yake nchini Afrika Kusini, hapa nchini ambapo iliudhuliwa na  viongozi wa kiserikali, dini,wajasiliamali, majaji, wasomi wa taaluma mbalimbali na wafanyabiashara.

Rais Mkapa alisema uzinduzi huo  GBR ambayo ni taasisi ya Kiikristo ambayo yenye lengo la kuwaunganisha binadamu wote wanao amini katika Mwenyezi Mungu ambao ni  wasomi wa taaluma mbalimbali, wafanyabiashara,serikali katika mataifa mbalimbali kuketi pamoja na kwamba watumia fursa na rasilimali walizopewa na Mwenyezi Mungu na taaluma zao waakikishe wanaweza kuleta maendeleo katika mataifa yao.

“Leo ni siku muhimu kwa Tanzania kwani Tanzania na leo imejiunga na kuanza kufanyakazi na GBR  ambayo moja ya malengo yake ni kuwaunganisha watu wote wanaomwamini Mwenyezi Mungu na ambao wanataaluma zao na wafanyabaishara kuungana pamoja kutumia fursa zilizopo kujiletea maendeleo ya kiuchumi wao wenyewe na mataifa yao….lakini mimi napenda niseme kuwa  nimefarijika na ujio wa GBR na niwaombe washiriki wote mtaoshiriki katika mkutano huu mjadili na muanishe ni mbinu gani zitumike kuinua hasa  sekta ya kilimo kwani kilimo ni biashara inayokuwa na  leo hii inaitaji wale wote wanaofanyabiashara katika sekta hiyo waweze na mbinu za kisasa,mitaji ya kueleweka na waweze kuuza bidhaa zao zinazotokana na kilimo kwa ngazi ya kimatifa”alisema Rais Mkapa.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo Kikuu cha Bagamoyo Profesa Costa Mahalu  alisema kwanza inatakiwa binadamu wote tupendane kama tunavyompenda mwenyezi Mungu na kwamba uzinduzi wa GBR hapa nchini  ,ambayo taasisi hiyo ina matawi yake nchi 12 sasa kutawasaidia kuwaunganisha pamoja watanzania na mataifa mengine kuweza kutumia rasilimali zilizowekwa na Mungu kwenye ardhi za nchi zao kuweza kusaidiana ili wote waweze kufikia  ngazi ya juu ya maendeleo kwani Mungu amependi watu wake waishi maisha ya ufukara.

Naye Balozi wa Heshima nchini Malawi ambaye ni Mkurugenzi Mstaafu wa Kituo cha Uwekezaji Nchini(TIC), Emmanuel Ole Naiko  alisema uwekezaji unaweza kufanywa na mtu yoyote yule na kwamba ujio wa GBR hapa nchini, ni faida kubwa kwa watanzania kuweza kuungana na mataifa mengine kujiletea maendeleo na kukuza uchumi wa biashara zao.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Alhamis, Agosti 15 mwaka 2013.


No comments:

Powered by Blogger.