Header Ads

HUKUMU KESI YA JERRY MURRO LEO

Na Happiness Katabazi


HAKIMU Mkazi wa Mkazi ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, Frank Moshi leo anatarajia kuketi kwenye kiti cha enzi na kumsomea hukumu aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la Taifa(TBC 1),Jerry Murro(30) na wenzake wanaokabiliwa na kesi ya kula njama na kuomba rushwa ya shilingi milioni 10.




Kusomwa kwa hukumu hiyo leo hii kunatokana na amri iliyotolewa na Hakimu Moshi, Oktoba 31 mwaka huu mahakamani hapo ambapo siku hiyo kesi hiyo ilikuja kwaajili ya kutajwa na kupangiwa tarehe ya kusomwa hukumu ya kesi hiyo ambayo inasubiriwa kwa shahuku kubwa.

Februali 5 mwaka 2010, ndiyo siku ya kwanza washtaki
wa hao kufikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mirumbe ambapo Wakili Kiongozi wa Serikali Stanslaus Boniface ambapo alidai Murro anakabiliwa na makosa mawili ya kula njama na kuomba rushwa ya shilingi 10 toka kwa aliyekuwa Mhasibu wa Halmashauri ya Wilaya ya Bagamayo,Michael Karoli Wage.

Wakati Mugassa na Kapama wanakabiliwa mashtaka hayo kama yanayomkabili Murro na shtaka jingine la tatu ambalo ni la kujifanya wao ni maofisa wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa(TAKUKURU), jambo ambalo si la kweli.Na kwa kipindi chote hicho washtakiwa wapo nje kwa dhamana.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Novemba 30 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.