Header Ads

SUMATRA,HAWA WAENDESHA PIKIPIKI POSTA MPYA VIPI?



Na Happiness Katabazi


NAANZA kuandika mtazamo huu kwa kuwaomba radhi waendesha Pikipiki maarufu ‘Boda boda”wanaoendesha pikipiki hizo katikati ya jijini la Dar es Salaam,kwa lengo la kutoa huduma ya usafiri kwa abiria wanaopenda kutumia huduma hiyo.

Nasema nawaomba radhi kwakuwa mtazamo huu wa leo unaweza kuwakwaza kwa njia moja au nyingine kwasababu nafahamu fika nyie waendeshapikipiki mliofurika kwa kasi maeneo ya Posta Mpya na maeneo mingine ya katikati ya mji, mnatafuta riziki ili mkono uende kinywani.

Itakumbukwa kuwa ni Mamlaka ya Usafiri wa Majini na Nchi Kavu(SUMATRA), ilizipiga marufuku daladala(Hiace) maarufu kwa jina la Vipanya kuingia katikati ya mji na badala yake ikaruhusu madaladala makubwa (DCM)ndiyo yatakuwa na kibali cha kuingia katikati ya mji na kutoa huduma hiyo ya usafiri kwa abiria.

Kweli amri hiyo ilitekelezwa kwa vitendo na hadi sasa Vipanya havitoi huduma ya usafiri katikati ya mji na badala yake vipanya vimekuwa vikitoa huduma ya usafiri katika barabara ambazo haziingii katikati ya jiji.

Lakini cha kushangaza hivi sasa takribani miezi minne sasa sisi tunaofanyakazi maeneo ya Posta mpya, tumeshuhudia idadi kubwa ya waendeshapikipi wakitoa huduma ya usafiri wa pikipiki bila ya hata SUMATRA kuutangazia umma kuwa imeziruhusu pikipiki hizo kutoa huduma katika ya mji.

Na mbaya zaidi waendesha pikipiki hao wamekuwa waziegesha pikipiki hizo kwenye vituo vinavyopaki daladala hali inayoleta usumbufu mkubwa kwa abiria wanasuburi kupanda daladala na watembea kwa miguu na kufanya abiria washindwe kutofautisha kituo cha kusubiria daladaka ni kipi na kituo cha kusubilia pikipiki ni kipi?

Wakati waendesha pikipiki wakiendelea kutamalaki katikati ya mji,hatujasikia Sumatra ikiutaarifu umma kuwa huduma ya pikipiki ndiyo imekuwa mbadala wa daladala (Vipanya).

Sumatra basi jitokezeni muueleze umma kama ni kweli usafiri wa pikipiki ndiyo umekuwa mbadala wa vile Vipanya mlivyovipiga marufuku ili tuelewe, kwani huo ukimya wenu unatukera na mwisho wa siku utakuja kusababisha madhara kwa abiria wanaosubiri madaladala vituoni na wanatemba kwa miguu.

Kwa sababu hivi sasa tunachoona kwenye vituo vya mabasi ni mashindano ya kuporana wateja baina ya makonda wa daladala na waendesha pikipiki.

Na kama ni kweli pikipiki ndiyo zimeruhusiwa kuja kutoa huduma ya usafiri badala ya Vipanya, basi huu utakuwa ni uwendawazimu wa hali ya juu, kwani huwezi kukataza vipanya visiingie katikati ya mji kutoa huduma ya usafiri wakati kinauwezo wa kubeba abiria wengi kuliko hizo pikipiki halafu ukaruhusu pikipiki ndiyo zitoe huduma.

Ieleweke wazi Mtazamo huu hauna lengo la kuharibu biashara ya usafiri wa pikipiki la hasha, unalengo la kuhoji Je ni halali kukataza vipanya siingine katikati ya mji kutoa huduma ya usafiri ambapo vipanya hivyo vinauwezo wa kubeba abiria wengi kuliko pikipiki halafu mamlaka husika zikaruhusu pikipiki ndiyo ziingie katikati ya mji kutoa huduma hiyo ya usafiri tena bila abiria anayepanda pikipiki hapewi risiti?

Ifike mahala mamlaka husika za serikali ziache mzahaa katika utendaji kazi na zitimize majukumu yake kwa maslahi ya taifa hili na siyo ubabaishaji kama huu, kama mamlaka husika ilisema uwepo wa Vipanya katikati ya mji ni uchafu, iweje leo hii iruhusu pikipiki ndiyo ziingie katikati ya mji kutoa huduma hiyo ?

Hakuna ubishi kuwa madai kuwa waendesha pikipiki wengi hivi sasa hawana mafunzo ya kutosha kuhusu uendeshaji wa pikipiki hizo hali inayosababisha kila kukicha ajali za pikipiki kuongeza na kusababisha majeruhi wa ajali za pikipiki kuleta msongamano mkubwa pale Taasisi ya Mifupa(MOI) yanaongezeka.

Sasa kama hivyo ndiyo serikali imejipanga vipi kuakikisha inawashughulikia madereva uchwara wa pikipiki ili wasiweze kuendesha pikipiki hizo?

Nimalizie kwakusema kuwa kuna ulazima wa SUMATRA kutolea tamko kuwa limewaruhusu waendesha pikipiki kutoa huduma hiyo katikati ya mji na kama imewaruhusu basi waendesha pikipiki hao wawekewe utaratibu wa maalum ili tuweze kuitambua kuwa pikipiki hii iliyopakwa rangi fulani ubavu inafanya safari zake mfano Sinza hadi Posta na abiria wanaotumia usafiri huo wapewe risiti na waendesha pikipiki hao wapangiwe kiwango cha nauli cha kuwatoza abiria hao.

Kinyume cha hapo utakuwa ni uwendawazimu tu uliowekewa baraka za mamlaka husika inayoshughulika na huduma ya usafiri mjini.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika.

0716 774494
www.katabazihappy.blogspot.com

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne,Novemba mosi,mwaka 2011.

1 comment:

Anonymous said...

LgjXqx [url=http://nba27.webnode.cn]英超赛程表[/url] PnlVam [url=http://nba28.webnode.cn]腾讯NBA直播视频[/url] MbjHti [url=http://nba29.webnode.cn]腾讯NBA直播视频[/url] FriDal [url=http://nba30.webnode.cn]新浪NBA直播[/url] LnvIqs [url=http://nba31.webnode.cn]天下足球直播[/url] IgwCur [url=http://nba32.webnode.cn]新浪体育NBA直播[/url] UodLev [url=http://nba33.webnode.cn]NBA直播视频直播[/url] YgnUgo [url=http://nba34.webnode.cn]NBA直播热火[/url]
UozMrn [url=http://nba35.webnode.cn]NBA直播视频直播[/url] KqlPmd [url=http://nba36.webnode.cn]新浪体育NBA直播[/url] DvyFdy [url=http://nba37.webnode.cn]吻球网足球直播[/url] LreUcv [url=http://nba38.webnode.cn]NBA直播[/url] SquJlz [url=http://nba39.webnode.cn]腾讯NBA直播[/url] BqkVse [url=http://nba40.webnode.cn]NBA直播视频直播[/url] MhwUfd [url=http://nba41.webnode.cn]英超赛程表[/url] TezWuv [url=http://nba421.webnode.cn]英超直播[/url]

[url=http://tt5252.com/]博彩网[/url]
MuzYqs [url=http://nba115.webnode.cn]足球直播[/url]QbpQtk [url=http://nba12.webnode.cn]英超赛程表[/url]KyqEqs [url=http://nba13.webnode.cn]风云足球直播[/url]EjpNkm [url=http://nba14.webnode.cn]NBA直播热火[/url]MguXuz [url=http://nba15.webnode.cn]吻球网足球直播[/url]HuiMhm [url=http://nba16.webnode.cn]英超赛程表[/url]AtrMxn [url=http://nba170.webnode.cn]腾讯NBA直播[/url]GfkCia [url=http://nba18.webnode.cn]英超赛程表[/url]
[url=http://tt2929.com/]太阳城娱乐城[/url]
ArhDvg [url=http://nba197.webnode.cn]NBA直播[/url] KccXqi [url=http://nba20.webnode.cn]天下足球直播[/url] LoiSug [url=http://nba21.webnode.cn]天下足球直播[/url] MnjLdp [url=http://nba22.webnode.cn]NBA直播表[/url] XdnQiy [url=http://nba230.webnode.cn]腾讯NBA直播[/url] BgyOgy [url=http://nba249.webnode.cn]天下足球直播[/url] AokRhl [url=http://nba25.webnode.cn]吻球网足球直播[/url] KaeRzf [url=http://nba26.webnode.cn]天下足球直播[/url]

Powered by Blogger.