Header Ads

KESI YA ALHAJI MINTANGA:SHAHIDI:DAWA ZA KULEVYA ZILIKUTWA KWENYE BEGI LA BONDIA PETO MTAGWA



Na Happiness Katabazi


ALIYEKUWA Kocha wa timu ya Taifa ya Ngumi , Nassoro Michael Irenge aliyeachiliwa huru na Serikali ya Mauritius kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya , ameieleza Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kuwa dawa hizo zilikutwa na wanausalama zikiwa ndani ya begi la Bondia Petro Mutagwa.

Irenge ambaye ni shahidi wa upande wa Jamhuri aliingia nchini hapa wiki iliyopita akitokea kwenye gereza moja nchini Mauritius alikokuwa akishikiliwa kwa kosa tuhuma hizo , alitoa madai hayo jana wakati akitoa ushahidi wake mbele ya Jaji Dk.Fauz Twaibu katika kesi kesi ya kula njama na kusafirisha dawa za kulevya zenye uzito wa Kg 4.8 toka Tanzania kwenda Mauritus kukutwa na dawa za kulevya ambayo inamkabili Rais wa zamani wa Shirikisho la Ngumi Tanzania (TFB) Alhaji Shabani Mintanga anayetetewa na wakili Jerome Msemwa na Yassin Memba ilikuja kwaajili ya kuanza kusikilizwa.

Irenge ambani askari wa Jeshi la Wananchi Watanzania(JWTZ), pamoja na mabondia wawili, Patrick Emilian na Petro Mutagwa walikuwa wakishikiliwa nchini Mauritus kwa tuhuma za kukutwa na dawa za kulevya wakati walipokwenda kwenye mashindano ya Champion mwaka 2008 nchini humo.Bondia Mutagwa bado anashikiliwa nchini Mauritus wakati bondia Emilian na Irenge waliachiliwa huru na serikali hiyo.

Akiongozwa kutoa ushahidi wake na wakili wa Mwandamizi wa Serikali Pridence Rweyongeza ,Irenge ambaye ni shahidi wa pili katika kesi hiyo alidai kuwa msafara wao ulikuwa na mabondia wawili Mutagwa na Emuilian na kwamba bondia wa tatu Abdallah Kimwaga hakufanikiwa kusafiri kwasababu alikosa tiketi lakini akadai kuwa siku ya kuondoka Mintanga alimweleza kuwa katika msafara wao watakuwepo mashahabiki watatu na kwamba hao mashabiki ndiyo ndio walimdhamini Bondia Mutagwa.

Alidai kuwa wakiwa uwanjwa wa Ndege wa Mwalimu Julia Nyerere alionana na watu wengine watatu ambao ni Phiris Kesi, Nathaniel na Ali Msengwa ambao walijitambulisha kwake kuwa wao ni mashabiki ambao wanajiunga kwenye msafara wake, kama awali alivyokuwa ameishaelezwa na na Mintanga.

“Mheshimiwa jaji mimi na mabondia wangu tulipofika Mauritus tulilala chumba kimoja katika tuliyokuwa tumeandaliwa na wenyeji wetu lakini cha kushangaza kesho yake usiku walikuja askari kutugongea mlango kwa nguvu minikamtaka Mutagwa aende kuwafungulia mlango na baada ya kufungua mlango waliingia askari wakiwa na silaha na kutuambia kuanzia wakati huo tupo chini ya ulinzi na baadae wakawaingiza na wale mashahabiki wakiwa na begi ambalo walilifungua na kutoa dawa ambazo walisema ni za kulevya,” alidai.

Awali akihojiwa na wakili Msemwa , Irenge alidai kuwa begi lile lilikuwa limeandikwa jina la Bondia Mutagwa lakini wakati akihojiwa na Wakili Msemwa akisaidiana na Wakili Memba na kuoneshwa maelezo yake aliyoaandika Polisi, Irenge alidai kuwa begi lile liliandikwa Tanzania.

Aidha katika maelezo ya Irenge alidai kuwa mashahabiki wale walikiri kutenda kosa hilo na kwamba dawa hizo walikuwa wamezimeza tumboni.

Akijibu maswali ya wakili Msemwa, Irenge alieleza kuwa Muntanga kuwa dhidi ya tuhuma zinazomkabili akidai kuwa yeye hakuwahi kukaa naye na kupanga njama kutenda kosa hilo na kwamba Mintanga hakuwai kusafiri na timu hiyo.

Alidai kuwa ingawa walifanyiwa upekuzi mkali katika viwanja vya ndege Dar es Salaam, Nairobi Kenya walikopotia na Mautius ambako walivuliwa hata nguo, lakini hakuna katika msafara wake ambaye alikutwa na dawa au kitu chochote kisicho cha kawaida.

Kw upande wake shahidi wa kwanza Christopher Mutabarukwa ambaye alikuwa Makamu wa Rais wa BFT alisema kuwa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho hilo ambayo ndio huidhinisha watu wa kuambatana na timu haikuwahi kuwaidhinisha mashahabiki hao.

Hata hivyo akihojiwa na wakili wa Mintanga, Mutabarukwa alidai kuwa hajui lolote kuhusu mahali zilikokamatwa dawa hizo huko Mauritius, aliyewakamata wala waliokamatwa nazo.

Kesi hiyo itaendelea tena leo ambapo shahidi wa tatu upande wa mashtaka ataendelea kutoa ushahidi wake.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 15 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.