Header Ads

MSHTAKIW KESI YA 'SAMAKI WA MAGUFULI'AIBUA MAPYA

Na Happiness Katabazi


WAKALA wa Meli ya Tawariq 1, Zhao Qinj(41) ambayo inadaiwa kukamatwa kwenye ukanda wa bahari ya Hindi ya Serikali ya Tanzania ikivua bila leseni na kuharibu mazingira, ameileza Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kuwa meli hiyo iliingia nchini Kenya na Tanzania tayari ikiwa na Tani 110 za Samaki ambazo ilizivua kwenye eneo la bahari kuu ambalo halimilikiwi na nchi yoyote duniani.


Zhao ambaye pia ni raia wa China, alitoa maelezo hayo jana wakati alipokuwa akitoa utetezi wake mbele ya Jaji Agustine Mwarija huku akiongozwa na wakili wake Ibrahim Bendera kutoa utetezi wake ambapo alidai kuwa wamiliki wa meli hiyo ambao hakuwataja majina yake ndiyo waliompa jukumu ya kuitafutia leseni Meli ya Tawariq 1 hapa Tanzania ili ije kuvua samaki na kwamba walimteua yeye kuwa wakala wa meli hiyo, maombi ambayo aliyakubali na akayatekeleza kwa vitendo kupitia mamlaka husika za Kenya na Tanzania.

Mshtakiwa huyo alidai Septemba 22 mwaka 2009 aliiandika barua ya Idara ya Uvuvi ya Zanzibar akiomba meli ya Tawariq 1 iruhusiwe kuvua kwenye eneo la Ukanda wa Uchumi, kwa muda wa miezi mitatu na nakala ya ombi hilo naitoa kama kielelezo na Zanzibar ilikubali ombi hilo na kisha nikawajulisha wamiliki wa hiyo meli kwa njia ya mtandao ambapo wakati nawajulisha kuwa kibali hicho kimepatikana Meli ya Tawariq 1 ilikuwa katika eneo la Bahari Kuu ambalo eneo hilo halimilikiwi na nchi yoyote hapa duniani.

Alidai kuwa ilipofika Desemba 2008 wamiliki wa meli hiyo walimtaarifu wamewatuma manahodha wa tatu wa meli hiyo wanaotokeo katika eneo hilo Bahari Kuu kuja mjini Mombasa ambapo anaishi mshtakiwa huyo ili waje kuchukua kibali hicho na Januari 1 mwaka 2009 manahodha hao waliwasili kwenye bandari ya Mombasa na akawapatia kibali hiyo na kisha akawapandisha kwenye meli iitwayo Tuosoun kwaajili ya kuanza safari.

“Machi 8 mwaka 2009 ndiyo meli ya Tawariq 1 ilifika bandari ya Mombasa ikitokea eneo la Bahari Kuu na ndani ya meli hiyo kulikuwa na tani 110 za samaki ambazo zilitakiwa kusafirishwa nje na kwamba walinitajia tani hizo za samaki ili yeye kama wakala wa meli hiyo aweze kwenda kufanya bokingi ya makontena ya kuifadhia samaki hao na kuandaa ilani ya meli hiyo na bandari ya Mombasa iweze kufahamu meli hiyo imebeba mzigo wa uzito gani;

“Lakini Machi 9 mwaka 2009 nikiwa Nairobi nikapigiwa simu na nahodha wa meli hiyo ambaye ni mshtakiwa wa tisa,Hsu Shang Pao kuwa kuna meli nyekundu imezingira meli yao ya Tawariq 1 baharini na kuikataza meli yao isiende Mombasa bali meli hiyo iende Dar es Salaam, na kwamba yeye baada ya kupokea taarifa hizo Machi 10 mwaka huo, alilazimika kupanda ndege kutoka Mombasa kuelekeza Zanzibar na kisha akachukua boti ya Sea Bus na kuisha kuingia Marine Polisi ya Dar es Salaam na alipofika hapo akakutana na askari mmoja ambapo yeye alijitambulisha kwa askari huyo kuwa yeye ndiye wakala wa meli hiyo iliyokamatwa”alidai Zhao.

Kesi hiyo imearishwa hadi leo ambapo washtakiwa wengine wataendelea kutoa utetezi wao.Mbali za Zhao washtakiwa wengine ni manahodha wa meli hiyo Hsu Shang Pao na Ca’ Dong Li na Chen Rui Hai.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima, Novemba 15 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.