Header Ads

WAZIRI AONGEZA MUDA KESI YA MBATIA,MDEE

Na Happiness Katabazi


HATIMAYE Waziri wa Katiba na Sheria Celina Kombani ameongeza muda wa miezi sita kuanzia jana katika kesi ya kupinga matokeo yaliyomtangaza mbunge wa Jimbo la Kawe, Halima Mdee(Chadema), kuwa mshindi kama alivyokuwa ametakiwa na Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, kuongeza muda huo.


Kesi hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu mwaka 2010 iliyofunguliwa na aliyekuwa Mgombea Ubunge kwa tiketi ya (NCCR-Mageuzi), James Mbatia anayetetewa na wakiliwa Mohamed Tibanyendera dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Mdee na Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Kawe.

Hayo yalisemwa jana na Jaji John Utamwa jana wakati kesi hiyo ilipokuja kwaajili ya kutajwa na kuangalia kama waziri huyo tayari ameishatekeleza amri hiyo ya mahakama ya kuongeza muda wa usikilizwaji wa kesi hiyo kwasababu kwa mujibu wa sheria ya Uchaguzi inataka kesi yoyote ya uchaguzi iwe imemalizika ndani ya miezi 12 , na kesi hiyo ya Mbatia na Mdee anayetetewa na Edson Mbogoro muda wa miezi 12 imeishapita na bado haijamalizika.

Jaji Utamwa alisema kwakuwa tayari muda umeishaongezwa, maelezo ya awali yatasomwa mahakamani hapo Desemba 6 mwaka huu na kwamba kesi hiyo itaanza kusikilizwa rasmi kuanzia Februali 7-10 mwakani.

Novemba 25 mwaka 2010, Mbatia alifungua kesi hiyo ya kupinga matokeo ya ubunge wa jimbo hilo ambayo yalimtangaza Halima Mdee(CHADEMA) kuwa mshindi.

Na kwa mujibu wa hati yake ya madai, Mbatia anadai kuwa katika mikutano ya kampeni, Mdee alimwita yeye kuwa ni fataki anayefanya mapenzi na watoto wa shule, kibaraka wa CCM na kila wiki analipwa sh milioni 80 na chama hicho, hivyo kuwataka wapiga kura wa jimbo la Kawe wasimchague Mbatia.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 29 mwaka 2011.

No comments:

Powered by Blogger.