Header Ads

DPP ASHINDA RUFAA KESI YA RICHMOND





Na Happiness Katabazi
MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dar es Salaam, imeufuta uamuzi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Saalam, uliomuona Mkurugenzi wa kampuni ya Richmond Ltd, Naeem Adam Gire aliyekuwa akikabiliwa na makosa ya kughushi,kuwasilisha nyaraka za uongo na kutoa taarifa za uongo kwa maofisa wa umma kuwa wana kesi ya kujibu.

Hukumu hiyo ilitolewa kutoka na rufaa Na.126/2001 iliyokatwa na  Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP), Dk.Eliezer Feleshi dhidi ya  uamuzi wa kesi ya kutoa taarifa za uongo kwa Shirika la Umeme la Tanesco Na. 15/2009 iliyokuwa ikimkabili Gire ambapo mwaka juzi Hakimu Mkazi Waliarwande Lema alimuona hana kesi ya kujibu.

Hukumu hiyo ilitolewa na jaji Lawrance Kaduri ambaye katika hukumu yake hiyo amesema asikiliza hoja za mawakili wa serikali waliokuwa wakimwakilisha  mwomba rufaa (DPP), Fredrick Manyanda na Oswald Tibabyekomya na mjibu rufaa alikuwa akiwakilishwa na wakili wa kujitegemea Alex Mgongolwa.

‘Baada ya kusikiliza hoja zote mbili na pia nimeangalia nakala ya uamuzi wa mahakama ya kisutu uliomwachiria huru Gire kwa maelezo kuwa hana kesi ya kujibu, mahakama hii imefikia uamuzi wa kuufuta uamuzi huo kwasababu imebaini kuwa kulikuwa na ushahidi wa kutosha ulioletwa na upande wa jamhuri kule katika Mahakama ya Kisutu ambapo umejitosheleza kumfanya Gire apande kizimbani na aanze kujitetea”alisema Jaji Kaduri.

Jaji Kaduri alisema anakubaliana na hoja za wakili wa Tibabyekomya iliyodai kuwa Hakimu Lema alikosea kisheria katika uamuzi wake alisema kuwa kosa la kughushi limeshindwa kuthibitika uamuzi ambao jaji huyo alisema hakimu Lema alisema alitumia sheria ambayo ilishapitwa na wakati kwa kusema kosa la kughushi limeshindwa kuthibitika.

‘Alisema Gire anakabiliwa na kosa la kuwasilisha nyaraka za uongo hivyo ushahidi unaonyesha Gire  aliwasilisha    
 Alisema kwa mujibu wa hati ya mashitaka kosa hilo la kughushi ,Gire anadaiwa kulitenda Machi 13 mwaka 2006 Dar es Salaam, kwania ya ovu  alighushi nguvu ya kisheria(Power of Attoney)ya Machi 13 mwaka 2006  kwa lengo la kuonyesha  Mohamed Gire  ambaye ni Mwenyekiti  wa Kampuni ya Richmond  Development  Company LLC ya Texa America amesaini hati ya nguvu ya kisheria  inayompa mamlaka  Naeem Adam Gire (Mjibu Rufaa) wa hapa jijijini  kuendelea na shughuli za kibiashara za kampuni hiyo hapa nchini kosa ambalo ni kinyume na kifungu cha 335(d) (iii) cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu ya mwaka 2002.

“Hivyo basi mahakama hii inakubaliana na mawakili wa mwomba rufaa(DPP), kuwa kosa hilo la kughushi hati ya nguvu ya kisheria liliweza kuthibitishwa na upande wa jamhuri hivyo mahakama hii inatamka wazi Hakimu Lema alikosea kisheria kusema upande wa jamhuri ulishindwa kuthibitisha kosa la kughushia hati ya nguvu za kisheria na kuwasilisha nyaraka hiyo hiyo ambayo ilighushiwa kwa maofisa wa umma kwa lengo la kuonyesha kampuni hiyo ilikuwa na uwezo wa kuzalisha umeme hapa nchini wakati si kweli ili wapewe zabuni’alisema Jaji Kaduri.

Aidha Jaji Kaduri alisema mahakama yake imejiridhisha kuwa kosa la kwanza na la pili(Kughushi na kuwasilisha nyaraka za uongo) limeweza kuthibitishwa na upande wa jamhuri, hivyo mahakama yake inaamuru kesi  ya msingi iliyokuwa imemalizika kwa Gire kuwaachiliwa huru baada ya kuonekana hana kesi ya kujibu, irudi upya katika Mahakama ya Kisutu na Gire anaanze kujitetea.

Mwaka juzi, Hakimu Mkazi wa mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Waliandware Lema alimwachilia huru Gire baada ya kumuona hana kesi ya kujibu na hakimu huyo alikwenda mbali zaidi na kusema upande wa jamhuri uache kufungua kesi kwa kukurupuka na kwamba mwisho wa siku mahakama inapowaachiria huru washitakiwa, matokeo yake mahakama inakuja kubebeshwa lawama.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Mei 17 mwaka 2013.

No comments:

Powered by Blogger.