Header Ads

MENEJA BENKI YA ACCESS KORTINI KWA WIZI

Na Happiness Katabazi
MENEJA wa Benki Access, Fadhil Muzo na maofisa wa mikopo wa benki hiyo wamefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam, wakikabiliwa na makosa ya wizi na uharibifu wa mali zenye thamani ya zaidi ya Sh.milioni 45,246,600.
 
Wakili wa Serikali Hilda Kato mbele ya Hakimu Mkazi Aniseth Wambura alidai kuwa mbali ya Muzo washitakiwa wengine ni  Michael Ntinga,Luka Tumbuka  ambao ni maofisa mikopo na Issack Nchembi ambaye ni dereva na kwamba wote wanakabiliwa na jumla ya makosa matatu.
 
Wakili Kato alilitaja kosa la kwanza kuwa ni la kula njama, kosa la pili ni la wizi  ambalo walilitenda Januari 29 mwaka  huu, katika eneo la Manzese jijini ambao waliiba  bidhaa mbalimbali ikiwemo  kreti za soda 31,katoni moja ya soda, katoni  53 za maji ya uhai, kreti  11 za bia aina ya Serengeti,katoni nne za bia aina ya Tusker, zenye jumla ya thamani ya Sh 45,246,600 mnali ya Rahamat Rashid Mandali.
 
Wakili Kato alilitaja kosa la tatu kuwa ni la uharibu wa mali ambalo walilitenda Januarui 29 mwaka huu, huko Manzese ambapo waliaribu Mlango wa ‘Gril’ wenye thamani y ash 250,000, mlango wa mbao wenye thamani ya Sh.90,000 na vishikizo vya kushikia mlango huo vitu vyote hivyo vina thamani ya Sh. 420,500 mali ya Wilbert  Makishe.
 
Na wakili Kato alidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na kwamba wanaomba mahakama iwapangie tarehe ya kuja kuwasomea maelezo ya awali.
 
Hata hivyo washitakiwa hao walikana mashitaka na walitimiza masharti ya dhamana yaliyomtaka kila mshitakiwa asaini bondi ya Sh.milioni nne.
 
Kwa upande wake Hakimu Wambura aliairisha kesi hiyo Juni 24 mwaka huu, kesi hiyo itakapokuja kwaajili ya upande wa jamhuri kuwasomea maelezo ya awali washitakiwa.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumatano, Mei 29 mwaka 2013. 
 

No comments:

Powered by Blogger.