Header Ads

NAENDELEA KUMLILIA WAKILI STANSLAUS BONIFACE 'JEMBE'






Na Happiness Katabazi
Leo  Mei 27 mwaka  2013, mpendwa wetu  aliyekuwa Wakili Kiongozi wa Serikali mwenye  cheo cha Mkurugenzi  Msaidizi wa ofisi ya Mkurugenzi wa Mashitaka nchini, Stanslaus Boniface Makulilo (44) ‘Jembe’ afariki ghafla  tarehe kama ya leo katika  Hospitali ya Regency jijini Dar es Salaam.

Binafsi mimi na wengine wote tunaoheshimu mchango wako wa Taaluma ya sheria uliyokuwa ukiiutoa kwenye mashauri mbalimbali yaliyokuwa yakiendeshwa katika mahakama mbalimbali hapa nchini, na wale mawakili wa serikali uliokuwa ukiwafundisha kazi tunaendelea kukumbuka na kukuenzi.

Na ndiyo maana leo hii mimi binafsi nikiwa Mwandishi wa Habari za Mahakamani na mwanafunzi wa  mwaka wa pili wa fani ya Sheria,ndiyo maana nimechukua muda wangu na  na ndiyo maana hata leo hii nimeweza kuchukua muda wangu na kuketi kitako na kuandika makala hii ya kumbukumbu ya mwaka mmoja ya kifo chako, na kukusimulia ni kesi gani za jinai kubwa zilifunguliwa na Mkurugenzi wa Mashitaka nchini DPP-Dk.Eliezer Feleshi na vijana wako uliowafundisha kazi waliweza kuziendesha kikamilifu na wakafanikiwa kushinda na nyingine wakashindwa na kesi nyingine ulizoziacha nyingine zimeishatolewa hukumu na nyingine bado.

Nianze kwa kukusimulia kesi kubwa kufunguliwa baada yaw ewe kufariki ni kesi ya uhujumu uchumi na madai ya kupokea rushwa inayomkabili Waziri wazamani Idd Simba na wenzake.Kesi hii ilifunguliwa rasmi  siku ambayo wewe Boniface ulikuwa unazikwa pale katika Makaburi ya Kinondoni  na ilikuwa ni Mei 29 mwaka jana, na hadi sasa bado haijaanza kusikilizwa.

Lakini pia Oktoba 18 mwaka jana, Dpp alimfungulia kesi wizi wa malighafi za Sh.milioni 59 na uchochezi Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Shaikh Ponda Issa Ponda na wenzake 49. Na DPP aliwasilisha hati ya kumfungia dhamana Ponda na Mkadamu Abdalah na kweli walisota gerezani hadi kesi hiyo ilipotolewa hukumu Mei 9 mwaka huu, ambapo Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Victoria Nongwa alimpotia hatiani Ponda peke yake kwa kosa moja la kuingia kwa jiani katika kiwanja cha Markazi Chang’ombe na kuwaachiria washitakiwa wengine 49 kwa maelezo kuwa jamhuri imeshindwa kuthibitisha kesi dhidi yao na hivyo Hakimu Nongwa akaamuru Ponda kutumikia adhabu ya kifungo cha mwaka mmoja nje.

Kwa upande wa jamhuri katika kesi hii ulikuwa ukiwakilishwa na wakili mwandamizi wa serikali Tumaini Kweka ambaye kwasasa ni wazi amekuwa akitajwa tajwa na watu wanaomshuhudia wakati akiendesha mashauri mbalimbali ya jinai, kuwa anafuata nyayo za marehemu Boniface.

Kesi nyingine ni kesi ya wafusi 53 wa Sheikh Ponda ambayo ilikuwa ikiendeshwa kwa Hakimu Mkazi Sundi Fimbo, ambapo  Machi 21 mwaka huu, alitoa hukumu ya kuwafunga mwaka mmoja jela baada ya kuwatia hatiani kwa makosa ya kufanya mkusanyiko haramu na kukaidi amri ya jeshi la polisi iliyowataka watawanyike na wasiandamane kwenda ofisi ya DPP, kumshinika ampatie Ponda dhamana.

 Lakini pia Machi 20 mwaka huu, Jamhuri ilimfungulia kesi ya tuhama za ugaidi Mkurugenzi wa Ulinzi na Usalama wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema),Wilfred Lwakatare na Ludovick Joseph  lakini hata hivyo Lwakatare alikimbilia Mahakama Kuu kuomba mahakama hiyo iitishe jalada la kesi hiyo na ilipitie kuona kama DPP alikuwa sahihi kumfungulia mashitaka Lwakatare ya ugaidi Machi 18 na kisha Machi 20 asubuhi kuyafuta na kisha Machi 20 mchana kumfungulia tena kesi yenye makosa hay ohayo  ambapo Jaji Lawrence Kaduri katika uamuzi wake aliotuoa Mei 8 mwaka huu, alimfutia mashitaka matatu ya ugaidi Lwakatare na kumbakizia kosa moja la kula njama kutaka kumuua kwa sumu Mhariri Mtendaji wa Gazeti la Mwananchi Denis Msacky.

Lakini hata hivyo Mei 8 mwaka huu, Jaji Kaduri alitoa uamuzi wa maombi hayo ya Lwakatare ambapo alisema DPP alikuwa sahihi kufuta na kumfulia mashitaka hayo, ila jaji huyo pia akatoa uamuzi wa kumfutia jumla ya makosa matatu ya ugaidi.

Hata hivyo Mei 21 mwaka huu, DPP aliwasilisha ombi lake Mahakama ya Rufani nchini akiomba mahakama hiyo itengue uamuzi huo wa mahakama kuu wa kumfutia Lwakatare  mashitaka ya ugaidi na hadi sasa bado uongozi wa mahakama ya rufaa haujapanga tarehe wala majaji wa kuanza kusikiliza rufaa hiyo.Na kesi ya msingi ya Lwakatare inakuja leo katika mahakama ya Kisutu kwaajili ya kutajwa mbele ya hakimu Mkazi Alocye Katemana.Na tangu Machi 18 mwaka huu hadi leo Lwakatare bado wapo katika gereza la Segerea kwasababu kesi inayowakabili haina dhamana.

Lakini hata hivyo Boniface Mei mwaka huu, Jaji wa Mahakama Kuu, Dk.Faudhi Twaibu alitoa amri ya kutupilia mbali hoja za mawakili wa jamhuri uliokuwa ukiwakilishwa na Oswald Tibabyekomya katika ile rufaa yetu ya kupinga hukumu ya kesi ya madai ya kuomba rushwa iliyokuwa ikimkabili Jerry Murro ambapo upande wa jamhuri ulikuwa ukiomba mahakama hiyo itoe amri ya kesi hiyo ilirudishwe mahakama ya Kisutu ianze upya kwasababu mwenendo wa kesi hiyo hausomeki vizuri, lakini Jaji Twaib alisema anatupilia mbali ombi hilo na kwamba sababu za kufikia uamuzi huo ameziifadhi.
 Pia wakili Boniface Aprili mwaka huu, Jaji Kaduri wa Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, alikubali rufaa iliyokuwa imekatwa na DPP katika kesi ya kupinga uamuzi wa Hakimu MKazi wa Mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu,Waliarwande Lema ambapo ulimuona Kigogo wa Kampuni ya Richmond Naeem Gire hana kesi ya kujibu.

Jaji Kaduri katika hukumu yake hiyo alisema kulikuwa na ushahidi wa kutosha ambao unamfanya Gire apande kizimbani ajitetea na hivyo hakimu Lema alikosea na hivyo jaji huyo akaamuru Gire apande katika mahakama ya Kisutu naanze kujitetea na tayari uongozi wa mahakama ya Hakimu mkazi Kisutu umeishampangia hakimu Emilius 

Mchauru kuanza kusikiliza utetezi wa Gire Juni 6 mwaka huu.
Lakini hata hivyo tayari Gire ameishawasilisha hati ya kusudio la kukata rufaa katika Mahakama Kuu na kwamba anachosubiri ni uogozi wa mahakama kuu umpatie nakala ya hukumu hiyo ili aweze kuandaa hoja zake na kuziwasilisha katika mahakama ya rufaa ni nchini kupinga hukumu hiyo.

Kuhusu zile jumla ya kesi 11 za wizi katika akaunti za EPA katika Benki Kuu, ambazo wewe na mawakili wenzako mlikuwa mkiziendesha na hadi unakutwa na mauti uliweza kufanikiwa kushuhudia kesi moja ya EPA ya wizi wa sh.bilioni 1.3 iliyokuwa ikimkabili Rajabu Maranda na Farijala Hussein wakihukumiwa kwenda jela miaka mitano, na ulivyofariki pia tayari kuna hukumu za kesi mbili za EPA ambazo zinamhusisha Maranda ,Farijala na maofisa wa BOT watatu zilitolewa hukumu. Hivyo kesi nyingine za EPA zilizosalia bado haizajatolewa hukumu .

Ila zile kesi nne za EPA zinazomkabili mfanyabiashara maarufu Jeetu Patel  zilizofunguliwa Novemba 2008 bado hata shahidi mmoja wa upande wa jamhuri hawajaanza kupanda kizimbani kuanza kutosha ushahidi wake.

Hizo ni simulizi chache za baadhi ya kesi zilizovuta hisia katika jamii na sisi waandishi wa habari kwa kipindi hiki cha mwaka mmoja ambacho wewe haupo nasi duniani.Ila napenda nikuakikishie tu kuwa mawakili wa serikali bado wanatupatia ushirikiano wa kutosha sisi waandishi wa habari za mahakamani kama zamani.

Unakumbukwa na waandishi wa habari za mahakamani wenzangu Furaha Omary, Regina Kumba, Magai James, Tausi Ally, Faustine Kapama, Kulwa Mzee,Grace Gurisha, Frola Mwakasala ,Karama ,Hellen Mwango.

Lakini bado unakumbukwa na mawakili wenzako wa Serikali, Dk.Eliezer Feleshi, Biswalo Mganga, Malangwe Mchungahela, Sedekia Emphere,Fredrick Manyanda,Oswald Tibabyekomya, Lasdslaus Komanya, Tumaini Kweka, Ponsian Lukosi,Ben Lincoln,Arafa Msafiri, Timon Vitalis,Michael Lwena na wengine wengi.Ambao kwa kadri ya uwezo wao wafanya vizuri katika majukumu yao ya ueneshaji wa mashitaka, na wengi niliozungumza nao wanakushukuru kwa mchango wako wa kitaaluma kwani hukuwa mchoyo wa kuwafundisha kazi pale walipoitaji msaada huo.

Miongoni mwa kesi kubwa ambazo mimi binafsi nilimshuhudia  Marehemu Boniface  akiziendesha kwa zaidi ya miaka mitano katika mahakama mbalimbali hapa nchini sasa ni kesi ya wizi wa shilingi bilioni 1.8 katika EPA, iliyokuwa ikimkabili Kada wa CCM, Rajabu Maranda na Farijala Hussein ambapo mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Mei 23 mwaka juzi, iliwahukumu kwenda jela miaka mitano, kesi ya kula njama na kuomba rushwa ya shilingi milioni 10 iliyokuwa ikimkabili aliyekuwa Mtangazaji wa Shirika la Utangazaji la TBC, Jerry Murro na wenzake ambapo Murro alishinda kesi hiyo mwaka juzi.

Kesi  ya Kikatiba iliyofunguliwa na mfanyabishara Jayankumar Patel “Jeetu Patel’ na wenzake dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, DPP na Reginal Mengi iliyokuwa akitaka afutiwe kesi zake nne za EPA zilizopo katika mahakama ya Kisutu kwasababu Mengi alimuhukumu kabla ya hajahukumiwa na mahakama kwa sababu alimuita ni Fisadi Papa, ambapo Boniface alimwakilisha AG na DPP na aliibuka mshindi katika kesi hiyo.

 Kesi nyingine kubwa ambayo marehemu alikuwa akiziendesha ambazo bado hadi umauti unamkuta hazijatolewa hukumu ni ile ya mauji ya Ubungo Mataa ambayo inaendelewa kusikilizwa na Jaji Projestus Rugazia, rufaa ya kupinga hukumu ya mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu iliyomwona mfanyabiashara Naeem Gile ambayo inasikilizwa mbele ya Jaji Laurence Kaduri ambaye alikuwa akikabiliwa na makosa ya kutoa taarifa za uongo kuhusu kampuni ya kufua umeme ya Richmond LCC, kuwa hana kesi ya kujibu, rufaa ya kupinga hukumu ya mahakama ya Kisutu iliyomuona Jerry Murro hana hatia na kesi ya matumizi mabaya na kuisababishia serikali hasara ya shilingi bilioni 11.7 inayomkabili waliokuwa mawaziri wa Fedha na Nishati, Basil Mramba, Daniel Yona na Gray Mgonja ambapo kesi hii hivi sasa imefikia hatua ya Mramba kuendelea kujitetea

Boniface alizaliwa Februali 21 mwaka 1968 ameacha mke na watoto watatu, aliitimu shahaha ya kwanza ya Sheria mwaka 1995 na shahada ya pili ya sheria alimaliza mwaka 2008 katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Julai Mosi mwaka 1995 aliajiriwa rasmi katika ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali kama Wakili wa Serikali, ilipofika Oktoba Mosi mwaka 2006 alipandishwa cheo na kuwa Wakili wa Serikali Mwandamizi.Oktoba Mosi mwaka 2007 alipandishwa cheo tena na kuwa Wakili Kiongozi wa Serikali. 

Nyadhifa ambazo Boniface aliwahi kuzishika enzi za uhai wake ni kati ya mwaka 2003-2007 alikuwa ni Wakili wa Serikali Mfawidhi Mkoa wa Mbeya.Kati ya Mei 2007 na Oktoba 2010 alikuwa Wakili wa Serikali Mfawidhi Kanda ya Mwanza.Novemba 2009 hadi Novemba 2010 alikuwa Mwanasheria Mfawidhi wa Serikali mkoani Dar es Salaam. Kutokana na utendaji kazi wake mzuri ilipofika Desemba 2010 hadi mauti yanamkuta aliteuliwa kushika wadhifa wa Mkurugenzi Msaidizi wa Kitengo cha uendesha mashitaka na pia awaka Msimamizi wa uendeshaji kesi zenye maslahi kwa umma. Bwana alitoa na bwana ametwaa jina lake liimidiwe.

Leo umetimiza mwaka mmoja tangu Boniface ufariki dunia, naendelea kukulia.

Chanzo:www.katabazihappy.blogspot.com
Facebook:happy katabazi  ; Jumatatu,  Mei 27 mwaka 2013
0716 774494

No comments:

Powered by Blogger.