Header Ads

NHC GHOROFA SIO LAZIMA ZIJENGWE UBUNGO

Na Happiness Katabazi


IELEWEKE wazi kuwa si lengo langu kupingana na baadhi ya hatua za maendeleo zinazoendelewa kupigwa na Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), chini ya Mkurugenzi Mkuu Nehemiah Mchechu.



La hasha kwanza napongeza baadhi ya hatua za kimaendeleo zilizopigwa katika kipindi cha muda mfupi na NHC ikiwemo cha kuwaumbua adharani wadaiwa sugu, na pia mikakati yako ya kuwabana wadaiwa sugu hadi hivi sasa tunaona baadhi ya wapangaji wanaoishi kwenye nyumba hizo wameanza kufuata utaratibu wa kwenda kulipa kodi ya pango kila muda unapofika.

Na kwale wanaosikiliza Redio Clouds kikamilifu, watakuwa wameishalisikia liletangazo NHC linalovutia na kuacha maswali mengi kwa wasikilizaji ambalo limekuwa likiwataka watu wanaotaka kununua nyumba za kisasa zilizopo katikati ya mji, madhali nzuri ambazo wamezipa jina la Ubungo Residential.

Kwa mara ya kwanza niliposikiliza tango hilo ndani ya gari na wenzangu tulibaki tukijiuliza maswali yafuatayo kuwa hayo majengo yako wapi?Je yameishajengwa?yapo ubungo eneo gani ambalo mimi silifahamu?. Na ili kupata ukweli wa hilo nilimtafuta rafiki yangu mmoja anayeishi kwenye maghorofa ya Ubungo-NHC na kumuuliza kwa undani kuwa nimelisikia tango hilo je hayo majengo yapo eneo gani?

Ndiyo huyo rafiki yangu akaanza kunieleza kuwa kwanza hayo majengo hayajaanza hata kujengwa na yanajengwa katikati ya maeneo ya maegesho ya magari na njia ya wapitao kwa miguu ambayo yapo ndani maghorofa ya NHC-Ubungo.Kwakweli nilichoka kabisa na kuamua kwenda kutembelea eneo hilo.

Nilipofika nikakuta mabati yamezungushwa katika eneo hilo ambalo ni kati ya ghorofa na ghorofa za awali ambazo watu wanaishi tangu miaka ya 1970 hali inayosababisha wakazi wa maeneo hayo hivi sasa kukosa hewa ya kutosha , eneo la kuegesha magari yao na watembea kwa miguu kushindwa kupita katika eneo hilo kama zamani.

Baada ya kukutana na hali hiyo kwakweli nilijiuliza hivi kama kweli serikali inania ya dhati ya kupanua mji ni kwanini imeruhusu NHC ijenge majengo hayo katika eneo finfu kama lilele?

Kama kweli NHC imeona biashara ndiyo bora zaidi kuliko afya za watu ni kwanini isingeiomba serikali maeneo makubwa tu ikaenda kujenga nyumba zake hizo inazodai ni sasa kisasa ili watu wanaotaka kuzinunua waende kuzinunua na kwenda kuishi huko?

Ni serikali hii hii ya Rais Jakaya Kikwete ilituhadi kuwa itakuza michezo, sasa ni michezo gani inayokuza wakati maeneo ya wazi katika maghorofa ya NHC-Ubungo ambayo utumiwa na watoto wadogo kucheza michezo mbalimbali, leo hii yanachukuliwa na NHC na kubadilishwa matumuzi na matokeo yake kwasasa yanajengwa makazi ya watu?

Basi NHC kama haiyataki maghorofa yake ya zamani ya hapo Ubungo ambayo bado watu wanaishi na shirika hilo linaendelea kupokea kodi zao, ni vyema basi shirika hilo lingewataka wapangaji wake wote wanaoishi hapo waame ili maghorofa hayo yavunjwe na kisha shirika hilo ndiyo lije na ramani ya kujenga hayo majengo ya kisasa kwa nafasi zaidi?

Aiingii akilini kwa watu waliofika eneo hilo linalotaka kujengwa maghorofa hayo ambayo yanatangazwa kana kwamba tayari majengo hayo ujenzi wake umeishamalizika, kuona watu wakiendelea kuishi katika eneo hilo wakati ujenzi wa majengo hayo mapya tunayoambiwa ni ya kisasa ambayo eti yatakuwa na eneo kubwa la kuegesha magari lakini kwa watu tunaofahamu eneo hilo la maghorofa ya NHC-Ubungo tunaishia kuchekea moyoni, ukikaribia kuanza.

Tanzania bado ina maeneo mengi tu yanaitaji kuendelezwa ama na mtu mmoja mmoja, serikali yenyewe, wawekezaji au hata hilo shirika la nyumba NHC.Kwa hiyo siyo lazima NHC ijenge majengo hayo ya kisasa ndani ya eneo ya maghorofa ya NHC-Ubungo ambapo watu wanaishi na kwa ukweli kabisa maeneo yaliyosalia katika si vyema yangepaswa kujengwa maghofa mapya.

NHC achaneni na tamaa ya kupata fedha za chap chap, kama kweli NHC mmpo kwaajili ya kukikisha mnaisaidia wananchi wa taifa hili kupata nyumba za kuishi iwe kwa kuwapangisha au kujenga na kisha kuziua, ni vyema mngewasiliana na Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Makazi, Profesa Anna Tibaijuka awapatie maeneo makubwa tu ili muweze kujenga hayo majengo ya kisasa ambayo yatakuwa na hewa zaidi ya hasili kuliko ilivyo hivi sasa maghorofa hayo mnayokusudia kuyajenga pale Ubunge, wakazi wa maghorofa hayo ya kisasa watategemea zaidi hewa ya isiyo ya halisi kwa kulazimika kutumia AC na Feni.

Mungu ibariki Tanzania, Mungu ibariki Afrika

0716 774494

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Novemba 29 mwaka 2011.

7 comments:

Anonymous said...

Wow, this post is fastidious, my younger sister is analyzing these things,
thus I am going to inform her.

Also visit my web page ID 52380

Anonymous said...

I'm gone to say to my little brother, that he should also pay a quick visit this webpage on regular basis to take updated from latest news update.

Stop by my blog avg rebill total

Anonymous said...

It is perfect time to make some plans for the future and it's time to be happy. I've read this post and
if I could I wish to suggest you few interesting things or tips.
Perhaps you can write next articles referring to this
article. I want to read more things about it!

my web site - reseller web hosting plan

Anonymous said...

Its like you read my mind! You appear to know a lot about this, like you wrote the book in
it or something. I think that you could do with a few pics to drive the message home a bit, but instead of that, this is fantastic blog.
A great read. I will definitely be back.

My web-site - direct consolidated loan

Anonymous said...

Hello there, You've done a fantastic job. I'll
certainly digg it and personally suggest to my friends. I'm confident they'll
be benefited from this site.

Feel free to surf to my homepage: search engine optimisation tools

Anonymous said...

I like it whenever people get together and share thoughts.
Great blog, stick with it!

Look into my web blog :: free home based business

Anonymous said...

Нi there! ӏ could have swοrn Ι've visited this site before but after looking at some of the posts I realized it's new to me.
Regаrԁless, I'm definitely happy I found it and I'll be book-marking it аnd сhecking back frequеntly!


Mу web-site; african oil painting on sale

Powered by Blogger.