Header Ads

SERIKALI YATETEA ADHABU YA KIFO

Na Happiness Katabazi

UPANDE wa Serikali katika kesi ya Kikatiba ya Kupinga adhabu ya kifo iliyopo katika Mahakama ya Kuu Kanda ya Dar es Salaam, umepinga kufutwa kwa adhabu hiyo kwasababu adhabu hiyo haivunji Katiba ya nchi.

Mlalamikaji katika kesi hiyo namba 67/2008 ni Chama Cha Wanasheria Tanganyika(TLS), Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHRC),Sahringon-Tanzania Chapter dhidi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, ambao wanatetewa na mawakili wa kujitegema Alex Mgongolwa, Fulgence Masawe, Chacha Boke na Julias Rugazi.

Pingamizi hilo liliwasilishwa juzi na Mkurugenzi wa Haki za Binadamu katika ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Methew Mwaimu mbele ya jopo la majaji wa tatu wanaongozwa na Jaji Robert Makaramba, Razia Shehke na Projest Rugazia.

Kwa mujibu wa hoja za upande wa serikali zinadai kuwa wanaomba adhabu hiyo iendelee kutumika kama sheria za nchi na kwamba adhabu si ya kiudhalilishaji na kamwe haitwezi utu wa binadamu hivyo kuimba mahakama hiyo itupilie mbali kesi hiyo ambayo imefunguliwa na mlalamikaji.

Baada ya upande wa serikali kuwasilisha pingamizi hilo kesi hiyo ilialishwa hadi Julai 22 mwaka huu , ambapo kesi hiyo itakuja kwaajili ya kutajwa.

Kwa mujibu wa hati ya madai, walalamikaji wanaiomba mahakama hiyo itamke kuwa adhabu ya kunyongwa hadi kufa ni kinyume cha Ibara 4(2),12(2),13(1),13(6)a,d,e,14,26(2),64(5) na 107(a) za Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kwani inazalilisha utu wa binadamu ambao unakatwa katika Katiba.

Ombi la pili ni kwamba sheria husika ya adhabu hiyo inailazimisha mahakama inapomkuta mtu ana hatia ni lazima anyongwe na wala haitoa adhabu mbadala kwa mahakama wakati Katiba inasema kazi ya utoaji wa haki na adhabu zake ni kazi ya mahakama.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, April 28, 2009

No comments:

Powered by Blogger.