Header Ads

MAHANGA AMDAI MSEMAKWELI BIL.3/-

Na Happiness Katabazi

IKIWA ni wiki moja tangu Mwanaharakati Kainerugaba aanike orodha ya vigogo aliyodai wamegushi sifa za kuwa shahada ya uzamivu(PhD) NAIBU Waziri wa Kazi ,Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk.Makongoro Mahanga, amemfungulia kesi ya kashfa katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, akitaka alipwe fidia ya Sh bilioni tatu kwa kumkashfu.


Dk.Mahanga ambaye anatetewa na wakili wa kujitegemea Kennedy Fungamtama alifungua kesi hiyo jana mchana mahakamani hapo ambapo tayari kesi hiyo imewa namba 145 ya mwaka huu.Kwa mujibu wa hati ya madai ambayo Tanzania Daima ina nakala yake inaonyesha wadaiwa wengine ni Mwandishi wa Habari wa Gazeti la Nipashe Muhibu Saidi. Mkurugenzi Mtendaji wa gazeti hili na Kampuni ya The Guardian Limited.

Dk.Mahanga abnadai kuwa kwa mujibu wa mdaiwa wa kwanza (Msemakweli) kuwa Oktoba 18 mwaka huu, aliitisha mkutano na waandishi wa habari na kutoa taarifa za kumkashifu na gazeti la Nipashe likachapisha habari ukurasa wa mbele kwa maneno yafuatayo:

“Dk.Mahanga amegushi sifa za kuwa ana shahahada ya uzamivu(daktari wa falsafa)wakati hajawahi kusoma shahda hiyo wakati wowote na mahali popote duniaani’: maneno ambayo alidai ni ya uongo na yalikuwa na lengo ya kupindisha ukweli.

Alidai kuwa maneno yaliyotumika kwenye nukuu hiyo yameonyesha mlalamikaji(Mahanga) alighushi vyeti hivyo, ni mtu asiyemwaminifu na ni mkosaji katika mazingira hayo na astahili kuendelea kushikilia nafasi ya kisiasa katika ofisi ya umma na bunge.

Dk.Mahanga aliendelea kudai kuwa Oktoba 19 mwaka huu, mdaiwa wa pili, tatu, na wa nne walimkashfu kwa kuchapisha taarifa iliyotolewa na mdaiwa wa kwanza, katika ukurasa wa kwanza katika gazeti la NIPASHE toleo Na.ISSN.0856-5414 Na.05443 ambalo lilibandika picha ya mlalamikaji kwa kuchapisha habari iliyotolewa na mdaiwa wa kwanza kwa malengo ya kisiasa.

“Gazeti la NIPASHE linachapishwa hapa jijini na kusambazwa hapa nchini na nchi za Afrika Mashaki, hivyo naomba mahakama hii iliamuru gazeti hilo kuniomba radhi katika ukurasa wa mbele kwa uzito ule ule wa habari waliyoichapisha awali, izuie wadaiwa kuchapisha habari inayohusu mambo binafsi kuhusu mimi ,biashara zangu,kazi zake za kisiasa bila idhini yangu”alidai Dk.Mahanga.

Wiki iliyopita Msemakweli aliitisha mkutano wake na waandishi wa habari na kudai kuwa amefanya utafiti na kubaini mawaziri sita waligushhi vyeti vya taaluma.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne, Oktoba 27, 2009

No comments:

Powered by Blogger.