Header Ads

KESI NYINGINE YA JEETU YASIMAMISHWA

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, kwa mara ya tatu tena, jana imetoa amri ya kusimamisha kesi ya wizi wa sh bilionio 3.3 katika Akaunti ya Madeni ya Nje(EPA) inayomkabili mfanyabishara maarufu,Jayantkumar Chandubhai Patel, maarufu kwa jina la Jeetu Patel na wenzake wawili, hadi kesi ya Kikatiba iliyofunguliwa na washitakiwa hao Mahakama Kuu ya Tanzania itakapomalizika.

Uamuzi huo ulitolewa jana na Mahakimu Wakazi Richard Kabate na Samwel Karua ambao walisema wamekubalina na maombi ya wakili wa utetezi Mabere Marando na Martin Matunda , yaliyotaka mahakama hiyo itoe amri ya kusimamisha usikilizwa wa kesi hiyo hadio kesi ya kikatiba inayoendelea Mahakama Kuu itakapomalizika.

Akisoma uamuzi huo Hakimu Mkazi Richard Kabate alisema mahakama hiyo inatupilia mbali pingamizi la wakili wa serikali Timon Vitalis lilotaka mahakama hiyo itupilie mbali ombi hilo la utetezi kwasababu tamko lilotolewa na Mwenyekiti wa IPP, Reginard Mengi dhini ya washitakiwa halikuwa lilikuwa haliivurugi kesi hiyo kwasababu kesi hiyo ilikuwa bado haijaanza kuendeshwa mahakamani hapo.

Hakimu Kabate ambaye alisoma uamuzi huo huku akitumia mifano ya kesi mbalimbali alisema pingamizi hilo la serikali halina msingi kwasababu kisheria kesi yoyote inapokuwa imefunguliwa mahakamani uwa inaendeshwa hatua kwa hatu hivyo siyo kweli kesi hiyo ilikuwa hainza kusilizwa.

“Kwa sababu hiyo tunatupilia mbali pingamizi la serikali lilodai kesi hiyo bado haijaanza kusikilizwa kwasababu kwasababu sheria inasema kesi ikishafunguliwa taratibu zingine ndani ya kesi hiyo zinaendelea…tunasema kesi hii imekuwa ikiendelea mahakamani hapa na ndiyo mahakama upande wa mashitaka na serikali ulikuwa ukifika mahakamani hapa na kuwasilisha maombi yao mbalimbali mbele ya jopo hili, hivyo kusema kesi hii ilikuba bado haijafikia hatua ya kuanza kusikilizwa siyo kweli”alisema Kabate.

Alisema licha washitakiwa hao wameshitakiwa kwa kesi hiyo lakini wanayo haki ya kudai haki zao za Kikatiba pindi wanapoona zinavunjwa na kuongeza kuwa mahakama ya Kisutu haina mamlaka ya kuendelea kusikiliza kesi hiyo kwasababu tayari washitakiwa hao wameishafungua kesi ya kikatiba katika mahakama ya juu.

“Tunatoa amri ya kusimamisha kusikilizwa kwa kesi hii hadi kesi iliyofunguliwa wa shitakiwa katika mahakama ya juu itakapomalizika na tunaagiza jarada la kesi hii lipelekwe mahakama Kuu”alisema Kabate.

Juni 4 mwaka huu, Jeetu na wenzake walifungua kesi ya Kikatiba Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam, inayosikilizwa na jopo la majaji watu wanaongozwa na Jaji Kiongozi, Fakhi Jundu, Geofrey Shahidi na Semistocles Kaijage. inaendelea kusikilizwa ambapo upande wa walalamikaji na wadaiwa wameishawasilisha utetezi wao na imepangwa kuanza kusikilizwa Novemba 2 mwaka huu.

Katika kesi hiyo, Jeetu na wenzake wanamshitaki Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Reginald Mengi na Mkurugenzi wa Mashitaka (DPP) kwamba kwa nafasi zao walishindwa kutimiza wajibu wao kikamilifu baada ya mdaiwa wa pili (Mengi) kuwahukumu kupitia vyombo vya habari kabla ya kesi zao nne zilizofunguliwa katika Mahakama ya Kisutu kutolewa hukumu.

Jeetu na wenzake walifungua kesi hiyo ya kikatiba Na. 30 wakiomba Mahaka ma Kuu itoe tafsiri sahihi ya ibara 13, kifungu 4, 5 na 6 (b) cha Katiba ambacho kinatamka watu wote ni sawa mbele ya sheria na pia itafsiri ibara 13 (6) (b) inayosema mtu yeyote asichukuliwe ana hatia hadi pale mahakama itakapomkuta na hatia.

Kwa mujibu wa hati ya madai, walalamikaji hao wanadai kuwa wamefikia uamuzi huo wa kuiomba mahakama itoe tafsiri ya ibara hizo za katiba kwa kuwa wanaamini zimevunjwa na Mengi ambaye Aprili 23, mwaka huu, alitumia vyombo vya habari kuwahukumu kwa kuwaita ‘Mafisadi Papa’ wakati Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu inayosikiliza kesi zao haijatoa hukumu.

Uamuzi huo ni wa watatu kutolewa katika kipindi cha Oktoba mwaka huu, mahakama hiyo ilitoa amri ya kusimamishwa kuendelea kwa kesi ya wizi wa sh bilioni 9, kesi ya wizi wa sh 3.9 zinazowakali washitakiwa hao hadi kesi ya kikatiba iliyofunguliwa na washitakiwa hao itakapotolewa uamuzi.

Washitakiwa hao wanakabiliwa na kesi nne za wizi wa fedha katika Akaunti ya EPA katika Mahakama ya Kisutu ambazo zilifunguliwa Novemba mwaka jana. Mbali na Jeetu, washitakiwa wengine ni Devendra Vinodbhai Patel, Amit Nady na Ketan Chohan.

Wakati huo huo, Mahakamani hapo jana mahakimu wakazi Samwel Kalua na Elvin Mgeta waliarisha usikilizwaji wa kesi wizi Fedha za Akaunti ya Madeni ya Nje(EPA) Sh bilioni 3.8 inayomkabili wafanyabishara watatu Farijara Hussein, Rajabu Maranda,Ajay Somay na maofisa wa BoT, Iman Mwakosya, Ester Komu na Sophia Kalika hadi leo kwasabu mshitakiwa wa kwanza(Farijara) anasumbuliwa na ugonjwa figo.

Uamuzi huo wa kuairishwa ulitokana na ombi la wakili wa utetezi Majura Magafu ambaye aliiomba mahakama hiyo iairishe usikilizwaji huo jana kwasababu mteja wake jana asubuhi alifika katika viwanja hivyo vya mahakama ila alianza kujisikia kuugua ugonjwa huo la kulazimika kwenda hospitali ya Burhan kwaajili ya matibabu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumanne,Oktoba 27, 2009

No comments:

Powered by Blogger.