Header Ads

USHAHIDI KESI YA MAHALU KUTOLEWA KWA VIDEO

Na Happiness Katabazi

MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, imekubali ushahidi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Mahalu na mwenzake kwa njia ya video.

Mahakama hiyo imekubali ombi hilo baada ya Wakili wa Serikali, Ponsiani Lukosi, kuwasilisha ombi hilo na kuiomba mahakama iwape muda wa kuwasilianana na shahidi wake aliyepo nchini Italia, ili aweze kutoa ushahidi wake kwa njia hiyo.

Nakubaliana na ombi la upande wa mashtaka la kutaka shahidi wao atoe ushahidi wake kwa njia ya mawasiliano ya video; naahirisha kesi hii hadi Machi 26 mwaka huu na mahakama itahamia Tanzania Global Develepment Learning Center,” alisema Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa, Sivangilwa Mwangesi, anayesikiliza kesi hiyo.

Katika ombi jingine wakili huyo wa utetezi, aliomba mahakama hiyo ihamie nchini Italia mbayo kosa limetendeka na kuongeza kuwa ombi la kutaka shahidi wao atoe ushahidi kwa njia ya mawasiliano ya video ni muhimu.

Hata hivyo, Wakili Cuthbert Tenga, ambaye anayemtetea mshtakiwa wa pili, Grace Martin, alidai sheria za nchi zinataka shahidi afike mahakamani kutoa ushahidi wake na siyo kutumia njia ya mawasiliano ya video na kuiomba mahakama hiyo iuone upande wa mashtaka umeshindwa kuendelea kuleta mashahidi.

Januari 21 mwaka huu, Mwangesi wakati akiahirisha kesi hiyo ambayo siku hiyo ilishindwa kuendelea kusikilizwa baada ya upande wa mashtaka kushindwa kuleta mashahidi; alisema anaahirisha kesi hiyo kwa mara ya mwisho.

Januari mwaka 2007 ilidai mahakamani hapo kuwa Mahalu na Grace ambao walikuwa ni maofisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Italia, waliisababishia serikali hasara ya sh bilioni tatu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Februali 27 mwaka 2009

No comments:

Powered by Blogger.