Header Ads

SERIKALI YAFUNGA USHAHIDI KESI YA BALOZI MAHALU

Na Happiness Katabazi

BAADA ya kesi ya wizi wa Euro milioni 1.3 inayomkabili aliyekuwa Balozi wa Tanzania nchini Italia, Profesa Costa Ricky Mahalu na Meneja Utawala na Fedha, Grace Martin kuairishwa kwa muda mrefu na Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam, jana upande wa mashtaka ulitangaza rasmi kufungusha ushahidi wake.

Sambamba na hatua hiyo, jana Mhimili mahususi wa mahakama nchini uliandika historia mpya kwa kesi hiyo ya jinai namba 1/2007 kupokea ushahidi wa shahidi kwa njia ya video katika Kituo cha Mafunzo ya Maendeleo ya Dunia Tanzania (TGDLC) kilichopo katika Chuo cha Usimamizi wa Fedha (IFM).Ambapo shahidi alikuwa akitoa ushahidi wake kwa lugha ya Kiitaliano na kutafriliwa kwa lugha ya Kiswahili na mkalimani ambaye ni Paroko Kanisa Katoliki Boko, Evarist Lefiyo.

Wakili wa (Takukuru) Ponsian Lukosi na Joseph Ole walifikia umauzi wa kufunga ushahidi katika kesi yao baada ya Naibu Msajili wa Mahakama ya Rufaa Sivangilwa Mwangesi ambaye ndiye anasikiliza kesi hiyo kukataa ombi la mawakili hao wa mashtaka kuiomba mahakama hiyo iairishe kwa kipindi kifupi kesi hiyo ili waweze kuleta shahidi mmoja ambaye naye yupo nchini Italia.

“Baada ya maairisho ya muda mrefu katika kesi hii na ndipo maana Februali 26 mwaka huu, pale Kisutu nilitamka wazi kabisa kwamba lile lilikuwa ni aiirisho la mwisho kwahiyo upande wa mashtaka leo(jana)mnaomba nitoe tena aiirisho la mwisho nasema hivi ombi lenu silikubali kwani endapo nitalikubali mimi ndiyo nitakuwa nachelewesha kesi hii hivyo basi Lukosi unafunga ushahidi au nifunge mwenyewe ushahidi?” alisema Mwangesi kwa sauti ya ukali.

Ghafla Lukosi akajibu kwa unyeyekevu na kueleza kuwa atafunga mwenyewe. “Mheshimiwa nitafunga mwenyewe ushahidi hivyo leo sisi upande wa mashtaka katika kesi hii napenda kuiambia mahakama hii kuwa tumefunga ushahidi wetu” alidai Lukosi.

Aidha Mwangesi alisema April 16 mwaka huu, siku hiyo ni siku ambayo atatoa uamuzi wa aidha washtakiwa hao wawili wanakesi ya kujibu au la.

Shahidi wa pili katika kesi hiyo ambaye ni raia wa Italia ambaye pia Kamishna wa Viapo, Marco Pape ambaye jana alikuwa akimalizika kutoa ushahidi wake kwa njia ya video akiwa Italia, alidai kuwa licha ya yeye anatoa ushahidi wake ushahidi mahakama wala Wizaira ya Mambo ya Nje ya Italia haijampa kibali cha kutoa ushahidi.

Pape ambaye jana alikuwa akimalizia kutoa ushahidi wake,alihojiwa na mawakili wa utetezi waliokuwa wakiongozwa na mawakili wa kujitegemea Mabere Marando, Alex Mgongolwa na Bob Makani,alidai kuwa taarifa za yeye kutakiwa kutoa ushahidi wake amezipata kwa Revocato Jojo na hata alipotakiwa na mawakili wa utetezi atoe ushahidi unaoonyeshwa kuwa aliitwa kutoa ushahidi alidai hana ushahidi huo kwa wakati ule bali ulikuwepo ofisini kwake.

“Sina ushahidi wa kuitwa kutoa ushahidi hapa ila ninao ofisini kwangu kwa Jojo alitumia kwa njia barua pepe ambapo alieleza leo(jana)natakiwa kutoa ushahidi kwa njia ya video katika kesi hii na hata hivyo ujumbe huo alionitumia hakuwa wa kikazi ulikuwa ni wa kibinafsi na hata leo ninavyotoa ushahidi huu najitolea silipiwi posha na mtu yoyote” alidai Pape.

Ifuatayo ni mahojiano katika wakili Mgongolwa na shahidi huyo;
Wakili:Mko wangapi katika chumba hicho unachotolea ushahidi?
Shahidi:Nipo peke yangu.
Wakili:Unaweza kutuambia chumba hicho kina ukubwa gani?
Shahidi:Mita tano kwa tatu.
Wakili:Shhahidi tukumbushe ulipokuja Dar es Salaam, kutoa ushahidi wako wa awali ulisema uliandaa orginal cell agreement, je wewe unayo?
Shahidi:Ninayo hapa.
Wakili:Ni orginal au photocopy?
Shahidi:Kwa mujibi wa Sheria za hapa Italia orginal inabaki kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali na mkataba kivuli unabaki kwa wakili husika.
Wakili:Shahidi ujaelewa swali unayo hapo au huna?
Shahidi:Sina.
Wakili:Uliwahi kushuhudia malipo ya mkataba wa nyumba hiyo ya ubalozi wetu hapo Italia?
Shahidi:Sikuona malipo wakati wanalipana.
Wakili:Kwa hiyo kwa maneno mengine wewe ujui walilipana kiasi gani?
Shahidi:Mimi ni mwanasheria kitaaluma kazi yangu ni kuandaa mkatana na kutia saini mambo ya malipo hayanihusu.
Wakili:Katika mahakama hii tuliambiwa malipo ya nyumba hiyo yalifanywa kwa njia Elektroniki, uliwahi kujua hiyo?
Shahidi:Nilisikia ila kimaandishi na kielektroniki sikuona hilo.
Wakili:Licha yaw ewe kuandika huo mkataba wewe uliwahi kuiona hilo jingo kwa macho yako?
Shahidi:Sijapata kuliona.
Wakili:Walipokuwa wanasaini huo mkataba wa ununuzi wa jingo hilo kuwaliwa na watu wangapi?
Shahidi:Nakumbuka Katibu wa Ubalozi alikuwepo na Balozi Mahalu.
Wakili:Unaweza kumkumbuka jina?
Shahidi:Simkumbuki jina.
Wakili:Mlikuwa wa ngapi?
Shahidi:Wanne au wa tano.
Wakili:Lwa maneno mingine ukumbuki idadi kamili?
Shahidi:Yes, sikumbuki idadi kamili.
Wakili:Baada ya kusaini huo mkataba nani alikuwa wa kwanza kutoka?
Shahidi:Mimi, nikawaacha wengine.
Wakili:Kwa hiyo tuchukulie wewe ni shahidi usiyeaminika kwasababu huna kumbukumbu?
Shahidi:Mwenye uamuzi wa mwisho ni hakimu.
Wakili:Tunachotaka uileze mahakama hii huna kumbukumbu sahihi za mkataba huo?
Shahidi:Mimi nina kumbukumbu kwa kila nilichoandika.

Ifuatayo ni mahojiano kati ya Bob Makani na shahidi Pape;
Wakili:Umetuambia baada ya kutia sani sikuile ulitoka?
Shahidi:Ndiyo nilitoka.
Wakili:Na ukarudi tena kwenye chumba kile mlichokuwa mkitiliana saini?
Wakili:Kwa hakika ndiyo nilirudi kwaajili ya kuwaaga.
Wakili:Kwanini ulirudi ukuwaaga wakati ulivyotoka?
Shahidi:Kwasababu wale walikuwa wanafanya taratibu za malipo na mimi nilivyotia saini nilitoka.
Wakili:Nasikia Waitaliano wanakwepa kodi?
Shahihi:Ndiyo lakini naamini hilo ni tatizo la duniano kote.
Wakili:Katika mtindo huo wa ukwepaji kodi,utashangaa ukiambiwa kulikuwa na mikataba miwili ambapo mkataba mmoja wewe ukuona?
Wakili:Sijaona mkataba mwingine.
Shahidi:Inawezekana kuwepo mikataba miwili mmoja ukaenda serikalini na mwingine ukabaki kwa mhusika?
Wakili:Inawezekana.
Makani:Ulijuaje unatakiwa kutoa ushahidi ?
Wakili:Wakili Jojo.
Wakili: Mahakama ya Italia imekupa kibali cha kutoa ushahidi hapo ulipo?
Shahidi:Hapana.
Wakili:Wizara ya Mambo ya Nje ya nchi yako imekuita kuja kutoa ushahidi katika kesi hii?
Shahidi:Hapana.
Wakili:Nani kakuita kutoa ushahidi?
Shahidi:Revocato Jojo.
Wakili:Mwambie Jojo akuonyeshe ushahidi wa wewe kuitwa kutoa ushahidi ?
Shahidi:Sina hapa, ninayo email yake ofisini.
Wakili:Alikutumia lini hiyo email?
Shahidi:Siku nne zilizopita.
Wakili:Je hiyo email ilikuwa ya kikazi au binafsi?
Shahidi:Email binafsi.
Wakili: Nani anakulipa kwa wewe kutoa ushahidi?
Shahidi:Najitolea, hakuna anayenilipa.

Ifuatayo ni mahojiano kati ya mawakili wa Takukuru, Ole na Lukosi kwa shahidi huyo;
Wakili:Shahidi ulipokea mikataba mingapi?
Shahidi: Mkataba mmoja
Wakili:Ulihusika na mkataba binafsi?
Shahidi:Hapana.
Wakili:Ulisani mkataba wa mauzo ya jengo la kiasi gani?
Shahidi: Euro milioni 1.3.
Wakili:Kwa mujibu wa sheria za Italia zinaruhusu kuwa na mkataba zaidi ya mmoja katika jengo moja?
Shahidi:Zinaruhusu mkataba mmoja tu.
Wakili:Mkataba halali ni upi?
Shahidi:Ni ule uliosainiwa adharani.
Wakili: Hawa washtakiwa wawili walikuwepo siku hiyo ya ya kutiwa saini mkataba?
Shahidi:Nakumbuka alikuwepo Profesa Mahalu wengine sina uhakika.

Awali kabla ya shahidi huyo kutoa ushahudi wake Mabere Marando kwaniaba ya jopo la upande wa utetezi, aliwalisha ombi la kupinga shahidi huyo kutoa ushahidi kwa njia ya video kwasababu Mahaka ya Hakimu Mkazi Kisutu haijapata kibali toka kwa Jaji Mkuu kusikiliza kesi nje ya mkoa wa Dar es Salaam, na kuongeza kuwa endapo Mwangesi atapokea ushahidi huo kwa njia ya video sheria za mipaka ya Italia.

Hata hivyo Mwangesi alilitupilia mbali pingamizi hilo na kuruhusu shahidi aanze kutoa ushahidi wake na Marando akaomba apatiwe mwenendo wa pingamizi hilo ili waweze kulipeleka Mahakama Kuu kwaajili ya mapitio ,ombi ambalo lilikubaliwa na Mwangesi ambapo alisema pindi mwenendo utakapochapwa watakabidhiliwa.

Januari mwaka 2007 ilidai mahakamani hapo kuwa Mahalu na Grace ambao walikuwa ni maofisa wa Ubalozi wa Tanzania nchini Italia, waliisababishia serikali hasara ya sh bilioni tatu.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Ijumaa, Machi 27 ,2009

No comments:

Powered by Blogger.