Header Ads

WANAHARAKATI WAFUNGUA KESI YA KUTETEA ALBINO

Na Happiness Katabazi

MASHIRIKA mawili yasiyokuwa ya kiserikali jana yalifungua kesi ya Kikatiba katika Mahakama Kuu Kanda ya Dar es Salaam dhidi ya Mwanasheria wa Serikali na wenzake kupinga ukiukwaji wa haki za binadamu unaofanywa kwa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino).

Mashirika hayo ni Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu(LHCR) na Chama cha Maalbino Tanzania ambao wanatetewa na mawakili Abdallah Possi,Nelly Gogley Moshi,Clarence Kipobota,Fredrick Mkatamba na Fulgence Massawe.

Kwa mujibu wa hati ya madai walalamikaji hao walidai kutokana na serikali kushindwa kuzuia mauaji hayo ni kukiuka Ibara ya 12(1),12(2),14,18(2) na 29(2) za katiba ya nchi.

“Kura za maoni zinaoendeshwa na serikali hazina nguvu ya kisheria kumkamata mtuhumiwa kwa vile anayeandika jina halazimishwi kutaja jina wala kuitwa mahakamani kama shahidi.
Aidha, katika kesi hiyo walalamikaji hao wanaiomba mahakama hiyo itoe amri ya kutungwa sheria itakayowezesha albino au walemavu kufurahia haki zilizoainishwa kwenye katiba ya nchi.

Chanzo:Gazeti la Tanzania Daima la Jumamosi, Machi 21 mwaka 2009

No comments:

Powered by Blogger.